Saturday, November 30, 2013

Watanzania changamkieni fursa hizi Burundi

Moja ya sababu kuu za kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ni kutoa wigo mpana wa soko na shughuli za kiuchumi miongoni mwa nchi wanachama.
Tanzania na Burundi ni kati ya nchi tano zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki. Nchi nyingine wanachama ni Kenya, Uganda na Rwanda, wakati nchi ya Sudan Kusini ikiwa imetuma maombi rasmi ya kujiunga.
Hivi karibuni, EAC iliandaa mafunzo ya siku tano kwa waandishi 25 wa Ukanda huo, mafunzo yaliyoambatana na mkutano wa pili wa siku tatu kuhusu Amani na Usalama miongoni mwa nchi wanachama.
Nilipata fursa ya kuwa kati ya waandishi watano waliowakilisha Tanzania kwenye mafunzo hayo yaliyolenga kuwanoa wanahabari namna ya kuandika habari za machafuko na migogoro bila kuleta madhara kwa jamii.
Pamoja na mafunzo, waandishi wa habari kutoka Tanzania walipata fursa ya kutembelea ubalozi wa Tanzania nchini Burundi. Walipata fursa ya kujifunza mambo kadhaa, mojawapo ni fursa za uwekezaji zinazopatikana nchini Burundi.
Katika mazungumzo yake na ujumbe wa waandishi wa habari kutoka Tanzania, Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dk James Mwasi Nzagi pamoja na mengine alizungumzia fursa ambazo Watanzania wanapaswa kuzichangamkia hivi sasa.
Uwekezaji katika sekta ya elimu, hasa lugha ya Kiswahili
Burundi ikiwa moja ya nchi zinazoongea lugha ya Kifaransa na Kirundi kama lugha rasmi ya kiofisi na mawasiliano, imeanza kutilia mkazo lugha za Kiswahili na Kiingereza ambazo ni lugha rasmi ya mawasiliano ndani ya EAC.
Serikali ya Burundi hivi sasa inahimiza wananchi wake kujifunza na kumudu lugha za Kiswahili na Kiingereza. Lugha hizo zinapaswa kufundishwa kuanzia elimu ya msingi, sekondari hadi Chuo Kikuu.
Katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania imekuwa ikizalisha idadi kubwa ya wahitimu katika sekta ya elimu kuanzia ngazi ya cheti, diploma na shahada.
 Balozi wa Tanzania nchini Burundi Dk. James Nzagi kushoto akiongea na waandishi wa habari kutoka Tanzania hivi karibuni.


Uzalishaji nishati ya umeme
Baada ya kumalizika kwa vita na machafuko, nchi ya Burundi hivi sasa inaelekeza nguvu nyingi kwenye kujenga na kuinua uchumi wa Taifa hilo kwa kuhimiza uwekezaji katika sekta ya viwanda, hasa vya uzalishaji.

No comments:

Post a Comment