Moja ya sababu kuu za kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki
(EAC), ni kutoa wigo mpana wa soko na shughuli za kiuchumi miongoni mwa
nchi wanachama.
Tanzania na Burundi ni kati ya nchi tano
zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki. Nchi nyingine wanachama ni
Kenya, Uganda na Rwanda, wakati nchi ya Sudan Kusini ikiwa imetuma
maombi rasmi ya kujiunga.
Hivi karibuni, EAC iliandaa mafunzo ya siku tano
kwa waandishi 25 wa Ukanda huo, mafunzo yaliyoambatana na mkutano wa
pili wa siku tatu kuhusu Amani na Usalama miongoni mwa nchi wanachama.
Nilipata fursa ya kuwa kati ya waandishi watano
waliowakilisha Tanzania kwenye mafunzo hayo yaliyolenga kuwanoa
wanahabari namna ya kuandika habari za machafuko na migogoro bila kuleta
madhara kwa jamii.
Pamoja na mafunzo, waandishi wa habari kutoka
Tanzania walipata fursa ya kutembelea ubalozi wa Tanzania nchini
Burundi. Walipata fursa ya kujifunza mambo kadhaa, mojawapo ni fursa za
uwekezaji zinazopatikana nchini Burundi.
Katika mazungumzo yake na ujumbe wa waandishi wa
habari kutoka Tanzania, Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dk James
Mwasi Nzagi pamoja na mengine alizungumzia fursa ambazo Watanzania
wanapaswa kuzichangamkia hivi sasa.
Uwekezaji katika sekta ya elimu, hasa lugha ya Kiswahili
Burundi ikiwa moja ya nchi zinazoongea lugha ya
Kifaransa na Kirundi kama lugha rasmi ya kiofisi na mawasiliano, imeanza
kutilia mkazo lugha za Kiswahili na Kiingereza ambazo ni lugha rasmi ya
mawasiliano ndani ya EAC.
Serikali ya Burundi hivi sasa inahimiza wananchi
wake kujifunza na kumudu lugha za Kiswahili na Kiingereza. Lugha hizo
zinapaswa kufundishwa kuanzia elimu ya msingi, sekondari hadi Chuo
Kikuu.
Katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania imekuwa
ikizalisha idadi kubwa ya wahitimu katika sekta ya elimu kuanzia ngazi
ya cheti, diploma na shahada.
Balozi wa Tanzania nchini Burundi Dk. James Nzagi kushoto akiongea na waandishi wa habari kutoka Tanzania hivi karibuni.
Uzalishaji nishati ya umeme
Uzalishaji nishati ya umeme
Baada ya kumalizika kwa vita na machafuko, nchi ya
Burundi hivi sasa inaelekeza nguvu nyingi kwenye kujenga na kuinua
uchumi wa Taifa hilo kwa kuhimiza uwekezaji katika sekta ya viwanda,
hasa vya uzalishaji.

No comments:
Post a Comment